Wednesday, January 25, 2017

Tafakari kwa Binti kabla ya kuolewa

#NDOTO_ZA_MABINTI_WENGI_NI_HARUSI.
Ukizungumza na wasichana au wanawake ambao hawajaolewa, unapozungumzia suala la Ndoa, kwa bahati mbaya sana wengi vichwani mwao inajengeka taswira ya harusi. Ukisema Ndoa yeye anawaza gauni jeupe (Shela) lenye mkia mrefu na maids wamelishika huku na huku. Anawaza suti ya mume wake, gari ya kifahari iliyopambwa, sijui wasindikizaji watoto pale mbele. Anawaza Ukumbini, baharini kupiga picha na mwisho usiku wa Honeymoon.
Ndio maana wengi wanakazana kuchangia harusi za wenzao na kushiriki hata kushona sare ili na yeye kwenye #HARUSI yake wamchangie.
Inasikitisha sana kwamba wengi hawafikirii maisha ya Ndoa.
Hawajiulizi maswali ya msingi kama;
=> JE NIKO TAYARI KUWA MKE WA MTU?
=> NIKO TAYARI KUJIDHABIHU KWAAJILI YA FURAHA YA MTU MWINGINE?
=> JE' NIKO TAYARI KUSALIMISHA MATAKWA YANGU KUFANYA MATAKWA YA MTU MWINGINE? (Surrendering my will)
=> JE' NIKO TAYARI KUWA MAMA NA KULEA FAMILIA?
=> JE' NIKO TAYARI KUPIGANIA NDOTO ZA MTU MWINGINE?
=> JE' NIKO TAYARI KUAMBATA IKIBIDI KUHAMA MJI NINAOPENDA NA KWENDA KUISHI NISIKOPENDA ILI KUTIMIZA NDOTO YA MUME WANGU?
*Niko tayari kuingia ukoo mwingine na kuufanya kuwa ukoo wangu, watu wake wawe watu wangu na Mungu wao awe Mungu wangu?
*Ikitokea umeolewa na Mume wako akapata shida ghafla mfano Ugonjwa na akashindwa kutunza familia, una mbinu gani mbadala ya kuendesha maisha yenu mpaka atakapopona na kusimama tena?
*Una uwezo wa kubeba majukumu kama Mama maana kuzaa ni jukumu lingine kabisa?
*Tabia yako vipi? Inafaa kuwa mke wa mtu? Au unahitaji muda kwanza na uhuru ujirushe ukichoka ndio utulie uolewe?
*Kuna msemo "Nyuma ya kila mwanaume aliyefanikiwa kuna mwanamke" ukijiangalia wewe una uwezo wa kumshauri mtu akafanikiwa? Na hilo tunalipima kwa kuangalia ni nini ambacho binafsi umefanikisha katika maisha yako.
*Moja jumlisha moja huzaa mbili, wewe una moja gani ya kuchanganya na moja aliyonayo mume wako mkazalisha mafanukio? Au unaenda kuwa Mama wa Nyumbani na mzigo. Ulishwe, uvishwe, upewe kila kitu wakati hakuna unachozalisha?
Nadhani kuna mambo ya maana ya kufanya, kupanga na kujiandaa kabla hujawaza rangi ya harusi (Wedding colour), keki ya ngazi saba na hotel ya kwenda Honeymoon. Me nimemaliza.
Kwa usawa huu hakuna mwanaume anataka kuoa mzigo. Usije ukaishia kufurahia harusi na baada ya mwaka ukaanza kutafuta Washauri wa Ndoa.

Mwanamke akipenda amependa kweli

Mwanamke akipenda anapenda kweli!
Mwanamke akikupenda anakuwa na furaha, anakuwa anajivunia kuwa na wewe, na hujihisi furaha kuongea na wewe.
Hupenda awe rafiki wa rafiki zako na ndugu zako, uvipendavyo na yeye atavipenda, atabadilisha mtindo wake wa maisha kuendana na mtindo wako.
Haitajalisha ni kiasi gani utamuudhi, atakusamehe hata kabla hujamuomba msamaha, atachokifanya ni kusubiri tu umuombe msamaha kuthibitisha kama kweli umejutia kosa lako.
Atajaribu kuwa na wivu na atakulinda kwani atahitaji uwe wake, wake peke yake na sio ku share. Atawakataa wengine wote wanaomtongoza kwa sababu ameona kesho yake ipo mikononi mwako.
Haitajalisha ni kiasi gani uko mbali na yeye, atajilinda kwa ajili yako. Atalike na ku comment kila kitu unachoweka facebook hata kama ni cha kipuuzi (hahaahaa).
Atakujibu kwa wakati text zako either watsapp, za kawaida au inbox ya fb. Hatajali kama unampa pesa au laa, kama ni tajiri au laa kwa sababu lengo lake ni kujenga maisha na wewe na sio kupass time ameona potentials kwako.
Atakuonyesha marafiki zake na ndugu zake, kwa sababu anajivunia kuwa mpenzi wako.
Tafadhali sana, muangalie mwanamke huyo, moyo wake umejawa na mapenzi, anastahili kutunzwa na kupendwa kama almasi.
Lakini tatizo kubwa la hawa "wavulana" (baadhi yao) baada ya kumfanya akupende zaidi, baada ya kupoteza muda wake juu yako, baada ya kuwakataa wanaume wengine ambapo kimsingi wengine walikuwa tayari kumuoa, baada ya kumuacha akutambulishe kwa ndugu zake na marafiki sasa unamuacha, unamkataa kwa mbwembwe nyingi, unamuacha akiwa na maumivu na aibu kubwa kwamba atawaambia nini wazazi wake, ndugu na marafiki, atatambulisha wangapi?
Na akiulizwa yuko wapi yule uliyetutambulisha? Awajibu nini!? Ofcoz atakachofanya ni kuinamisha kichwa huku ameshika mashavu! Hana jibu ni aibu na maumivu makubwa kwa kuwa alikupenda kwa dhati.
Mbona mnawaweka katika wakati mgumu wanawake waliopewa moyo wa kupenda?
Brothers, usimfanye mwanamke wako ajute kwanini alipenda, usifanye wengine wamcheke na kumdhihaki. Timiza ahadi yako, kama amekukosea na kukuomba msamaha jaribu kumpa nafasi ya pili. Kila mtu anahitaji nafasi ya pili ili aweze kurekebisha pale alipokosea.
Na nyie vijamaa mnaokua sasa, miaka 14 na kuendelea msiige tabia ya sisi kaka zenu, hiyo sio tabia njema kabisa. Jifunzeni kuheshimu hisia za mtu. Kujeruhiwa kihisia kunauma kuliko maumivu ya risasi.
Kama huna future nae usimtongoze na kumpa mimba

Jinsi ya kujikinga dhidi ya magonjwa haya ya zinaa

Njia bora na ya uhakika zaidi kwa wasichana kujikinga dhidi ya maambukizo ya magonjwa ya ngono ni kuachana na ngono katika umri mdogo na kabla ya ndoa. Uelewa juu ya magonjwa haya pia ni njia inayosaidia katika mapambano.
Kwa wasichana ambao hawajaanza kujamiiana na wanaume, wanaweza kupewa chanjo ya kuzuia maambukizi ya virusi wanaosababisha ugonjwa wa saratani ya mlango wa mji wa mimba ambayo ni salama. Chanjo hii haiwasaidii wasichana ambao tayari wamekwishaanza tabia ya kujamiiana na wanaume katika umri mdogo kwa vile mara nyingi huwa wamekwisha pata maambukizi.
Njia pekee inayosaidia wasichana ambao wamekwishaanza kujihatarisha kwa kufanya ngono mapema, ni kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu katika vituo vya tiba za kisayansi ili kuona kuwa viashiria vya awali vya saratani vimeanza kujitokeza au la.
Uchunguzi huu hufanyika kwa kutumia kipimo cha mpako wa asidi ya Acetic na kuangalia - Viasual Inspection with Acetic Acid (VIA). Kama itagundulika kuwa msichana tayari amekwisha athirika kwa virusi hawa, atapatiwa matibabu kabla hajachelewa. Saratani ya mlango wa mji wa mimba inazuilika na kutibiwa kabisa iwapo itagunduliwa na kutibiwa mapema.
Tabia ya kuchangia nguo za kuvaa au taulo za kujifutia maji baada ya kuoga pia ikiepukwa, inasaidia kwa kiasi kikubwa katika kinga ya magonjwa haya. Magonjwa kama kaswende, kisonono, upele na mengine yanaweza kuambukizwa kwa urahisi kupitia njia hii ya kuchangia nguo, mavazi ya aina nyingine au matandiko.
Njia nyingine ya muhimu ni ile ya kuepuka vishawishi kutoka kwa wavulana na wanaume wasiojiheshimu. Vishawishi vya pesa, simu za mkononi, lifti za magari, vyakula kama viazi vya kukaanga maarufu kama chips na nyama ya kuku, mara nyingi hutumika kuwanasa wasichana wengi hasa wale wenye tamaa mbaya ya vitu na wenye uroho wa vyakula. Wengi husahau umuhimu wa maisha na masomo na huangalia vishawishi kama mafanikio, badala ya mtego yenye hatari kwa afya zao na maendeleo yao.
Kumbuka kuwa mazoea mabaya yakisitawishwa ni vigumu sana kuyaacha. Jitihada kubwa sana zinahitajika ili kuepuka mtego huu wa kufanya mapenzi na ngono katika umri mdogo. Jitahidi kwa kadri ya uwezo na nguvu zako zote za kimwili, kiroho na kiakili kupambana na hisia hasi kuelekea ngono hata kama ni vigumu, kwani huo ndio uamuzi sahihi na salama.
Jaza mawazo na hisia njema katika akili yako kila siku na kuepuka jambo lolote linalokupeleka katika mtego wa kuwazia mapenzi ya mahaba na ngono.Tamaa ya ngono inaweza kutawaliwa kwa mafanikio, kwani Mungu ameweka uwezo mkubwa ndani ya akili za wasichana ili waweze kujitawala. Na ushahidi wa jambo hili ni mwingi sana katika jamii za mataifa mbalimbali katika historia.
Epuka hadithi na liwaya za mahaba, magazeti ya udaku yanayosifia ngono, vipindi vya luninga (Televisheni) vinavyopamba mambo ya mapenzi na ngono kiufundi ili kuwavutia vijana. Epuka mitandao ya wavuti pamoja na mikanda ya video inayoonyesha picha za ngono na miziki inayochochea mapenzi na ngono. Nijambo la busara pia kuwaepuka marafiki pamoja na vijana wa rika lako wasiokuwa na maadili mema.
Wasichana wengi huondoa hofu na kujidanganya kuwa wanaweza kuonyeshana mapenzi na wavulana kwa kukumbatiana, kubusiana, kunyonyana ndimi na kushikanashikana sehemu za siri bila kufanya ngono. Hilo ni jambo la hatari, ni mbegu nzuri ambayo baada ya muda mfupi itazaa matunda ya ngono hatarishi.
Matendo hayo huamusha na kuchochea kwa nguvu sana hisia, tamaa mbaya na hamu kali ya ngono kwa wasichana na wavulana ambayo itawasumbua sana na baada ya muda mfupi sana watatumbukia ghafla katika mtego wa ngono hatarishi. Kanuni ya usalama ni kuepuka kuchezacheza na mambo ya hatari. Epuka kuchezacheza na bunduki yenye magazini iliyojaa risasi, kwani ni rahisi kufyatuka na kusababisha maafa makubwa.

Athari za magonjwa ya ngono kwa wasichana

Wasichana wengi wanaojihusisha na maswala ya ngono katika umri mdogo wanakabiliwa na ongezeko la uwezekano wa kupata saratani ya mlango wa mji wa mimba (cervical cancer). Shingo ya mlango wa mji wa mimba ambayo haijakomaa inapokutana na misukosuko ya ngono hudhoofika na kupoteza nguvu za kukabiliana na mashambulizi ya virus vya Human Papilloma – (HPV) ambao husababisha saratani hiyo mapema au baadaye sana.
Virusi hawa huambukiza kwa njia ya kujamiiana na wanaume hata kama mwanaume atakuwa amevaa kondomu wakati wa kufanya tendo la ngono na msichana. Saratani hii ni tatizo kubwa la kiafya linaloongoza kwa vifo vya wanawake vitokanavyo na ugonjwa wa saratani katika nchi zinazoendelea. Saratani hii kwa kawaida huwapata wanawake wengi ambao huanza kufanya tendo la kujamiiana katika umri mdogo, miaka michache baada ya kuvunja ungo.
Wasichana na wanawake wenye wapenzi wengi, au wenye wapenzi wa kiume ambao wana mtandao mkubwa wa wapenzi wengine wengi, huwa katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya virusi wanaosababisha ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi.
Kwa bahati mbaya sana wasichana wengi hupata maambukizi ya virusi hawa kwa kufanya ngono kwa mara ya kwanza, hata kama ni mara moja tu. Tatizo jingine kuhusiana na maambukizi ya virusi hawa ni kwamba, msichana anaweza kuishi na virusi hawa bila habari kwa miaka 10 hadi 15 hivi ndipo madhara yake yanapojitokeza kwa wazi.
Tatizo jingine linalowakabili wasichana wadogo wanaoendekeza ngono ni ugumba wakati watakapo hitaji kuzaa. Magonjwa mengi ya ngono hushambulia mirija ya uzazi na kusababisha mirija hiyo izibe. Mirija ya uzazi inapoziba, hushindwa kupitisha mayai kwa ajili ya kutunga mimba pale msichana atakapohitaji kupata watoto hapo baadaye.
Magonjwa ya ngono kwa wasichana pia husababisha maumivu makali na kuugua hasa pale tumbo la chini linaposhambuliwa. Msichana hupata ugonjwa wa mwanamimba yaani uambukizo katika mji wa mimba na wakati mwingine katika njia ya mkojo. Hii pia huambatana na maumivu makali wakati wa kukojoa.
Magonjwa mengine katika kundi hili la magonjwa mengi mbalimbali, husababisha madhara makubwa na ya muda mrefu. Kaswende inaweza kusababisha ugonjwa wa moyo na akili hasa pale msichana anapochelewa kupata matibabu sahihi. Magonjwa haya pia yanaweza kukaa mwilini kwa muda mrefu bila kuonyesha dalili huku yakiendelea kudhuru afya ya msichana.

Magonjwa yanayohusiana na tendo la ngono

Magonjwa ya ngono ni maambukizi yanayosambazwa kwa njia ya tendo la ngono au kujamiiana. Magonjwa haya kwa karne nyingi yamejulikana kama nyororo la maangamizi au bomu la kibaiolojia. Hii ni kutokana na ukweli kuwa ukiona mgonjwa mmoja mwenye tatizo la ugonjwa wa kuambukiza kwa njia ya ngono basi ni muhimu kutambua kuwa kuna mtu mwingine nyuma yake ambaye ana tatizo hilo pia.
Kwa kawaida wasichana huwa katika hatari kubwa zaidi ya kupata magonjwa ya ngono kama watajiingiza katika vitendo vya kujamiiana. Sababu kubwa zinazowaweka katika hatari ni ile hali ya kushindwa kuamua namna ya kufanya ngono kwa tahadhari, maumbile ya kike kama mpokeaji na kutokukomaa kwa shingo ya mji wa mimba nazo ni sababu zingine zinazoongeza hatari.
Magonjwa mengi ya ngono husababishwa na bakteria, virusi, kuvu (fungus), protozoa na parasaiti. Magonjwa yasababishwayo na bakteri ni kama vile kisonono, mitoki (Granuloma inguinale na Chancroid), kaswende na klamydia. Magonjwa kama vile malengelenge (Herpes simplex), molluscum contageosum, viotea (warts), virusi vya UKIMWI na saratani ya mlango wa kizazi (HPV infection) haya hutokana na virusi. Magonjwa yasababishwayo na kuvu ni kama vile kandidiasisi ambayo huambatana na muwasho sehemu za siri. Magonjwa yaletwayo na protozoa kama vile Trikomoniasisi pia husababisha muwasho sehemu za siri na hutokwa kwa majimaji machafu yenye harufu mbaya hasa kwa wanawake. Upele na chawa wanaokuwa kwenye nywele za kinenani haya pia ni magonjwa ya ngono yanayosababishwa na parasaiti.
Dalili za magonjwa ya ngono hujitokeza kwa njia na dalili nyingi. Wakati mwingine magonjwa haya hayatokezi dalili zozote na pia mgonjwa anaweza kupata maambukizo ya magonjwa mawili au zaidi kwa wakati mmoja anapotenda tendo la ngono. Hatari kubwa zaidi inayoambatana na magonjwa haya ni kutokuwepo kwa dawa zinazotibu baadhi ya magonjwa haya kama vile UKIMWI.

NGONO KABLA YA NDOA KWA MSICHANA

Siku hizi ngono kabla ya ndoa hutazamwa na vijana wengi kama jambo la kawaida.Vijana wa kike na wa kiume hawahisi hatia yoyote ya kuwa na uhusiano wa kingono katika umri mdogo. Kwa kufanya hivi vijana hupoteza mwelekeo kwa kuishi kiholela bila ya kuwa na mwongozo unaongoza maisha yenye mafanikio sasa na baadaye. Uwezo, fursa na bahati ya vijana kwa ajili ya maisha bora hupotea bure. Vijana hufikiria kuwa ngono ndilo jibu na ufumbuzi wa hali ngumu wanayokabiliana nayo wakati wa balehe na kupevuka. Wengi wao hupungukiwa uwezo wa kutabili nini kitatokea baadaye kama matokeo ya ngono kabla ya ndoa.
Wasichana wanaojiingiza katika mahusiano ya kingono kabla ya ndoa na katika umri mdogo huweka rehani uaminifu, afya na uvumilivu wao wa hisia kuhusu mahusiano ya kingono wakati watakapo ingia ndani ya ndoa hapo baadaye.Vijana wengi hawaelewi kuwa ngono haramu huzaa wivu, tuhuma mbaya na majanga ya kijamii. Hufanya mwenzi kumfikiria msichana kuwa ana udhaifu wa kimaadili na hali hii hutia alama katika hisia za mwenzi kuhusu hali ya uaminifu wa mwenzake hasa pale anapokuwa mbali naye.
Tafiti kadha wa kadha huonyesha kuwa wasichana wasiothamini umuhimu wa kujitunza, kujilinda na kubakia waaminifu kabla ya ndoa, wana uwezekano mara dufu wa kufanya ngono nje ya ndoa baada ya kuolewa ikilinganishwa na wale wanaojitunza na kuanza ngono ndani ya ndoa. Uzoefu pia unaonyesha kuwa wasichana wengi wanaoanza ngono kabla ya ndoa, maisha yao ya baadae huwa magumu kutokana na kuacha masomo au kuzaa hovyo ovyo bila mpangilio. Wengi hujikuta wakizaa na wanaume wengi tofautitofauti na kusababisha malezi ya watoto kuwa magumu.
Wasichana wengi hufikiri kuwa ngono kabla ya ndoa ndio njia pekee ya kujenga na kudumisha uhusiano wa kimapenzi na wavulana. Hii si kweli na huenda msichana na mvulana wanaotamaniana kingono hutazamana kwa mitazamo inayotofautiana kabisa mara baada ya tendo la ngono. Ni vigumu kutabiri nini kitatokea baada ya mvulana kutosheleza tamaa yake ya ngono kwa mara ya kwanza.
Huenda mvulana akamwona msichana havutii tena kimahaba na kumchukia sana. Huenda msichana pia akapata athari za kisaikolojia na kupata hisia za kunyanyaswa kijinsia au kutumiwa kama chombo cha kustarehesha wanaume kingono. Na huenda akajichukia kwa udhaifu na kujirahisisha aliko onesha. Hii mara nyingi hutokea pale msichana anapokataliwa na mvulana baada ya kupata mimba.
Mbali na athari za kisaikolojia na kijamii, ngono katika umri mdogo kabla ya ndoa pia inazo hatari za kiafya katika mwili wa msichana. Tishio kubwa kwa wasichana ni maambukizi ya magonjwa kama vile virusi vya UKIMWI, kansa ya mlango wa mji wa mimba na magonjwa mbalimbali yaambukizayo kwa njia ya ngono.

Maalum kwa kina Dada: Sheria 10 za Kumridhisha mwanaume wako kimapenzi!

http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/03/wowowo.jpg?x41673Mtaalam wa mapenzi, Bi. Layla Quinn, anasema wamaume ni viumbe rahisi sana kuridhishwa tunapokuja katika suala la unyumba. Mwanzoni, kitu kinachomhamasisha mwanaume kujamiiana ni muonekano wako (mwanamke) tu wakimahaba, lakini kadri siku zinavyokwenda ndani ya mahusiano, inakuwa ngumu kupandisha munkari wake, hata kama wewe ni mwanamke mrembo barabara!
Bi. Layla anaendelea kusema kuwa, kumridhisha mwanaume wako kitandani inaweza ikawa rahisi kama tu utakumbuka kuweka mambo katika hali ya mvuto ( Remember to keep things intereting!). Tafuta namna ya kuleta hamasa, iliyokuwepo siku za mwanzo mwanzo, na kwa hakika utakamata usukani. Sasa swali linakuja…..Nini unatakiwa kufanya, ili kumridhisha mwanaume wako kitandani? Kujibu swali hilo, Bi. Layla amekuja na sheria 10 zifuatazo, ambazo kama zitazingatiwa kwa makini, basi mwanamke hatokuwa na shida ya kumridhisha mwanaume wake kitandani na nyanja nyingine muhimu za mahaba.
# 1 Vaa vizuri. Utamu wa kujamiiana unaweza ukawa kwenye tendo lenyewe, lakini matamanio ya kufanya tendo hilo, yanategemeana na mambo mengine mengi. Vaa vizuri wakati wa kulala wakati wote, na sio tu wakati wa usiku, ambao unataka kufanya mapenzi. Vaa nguo nyororo, yenye mtelezo unaomwagika mwilini. Kwa vazi hili na mtembeo wa kimahaba chumbani, mwanaume wako hatotaka kutoa mikono yake mwilini mwako.
#2 Usiwe mtu wa aibu aibu linapokuja suala la kujamiiana. Mwaume anaweza akakupenda kwa mapozi yako na aibu kwanza (lugha iliyotumika hapa ni “innocence”), lakini hamna mwanaume atakaye endelea kuvumilia mwanamke, ambaye anastushwa kirahisi na kila kitu (mitindo ya kujamiiana), isipokuwa mtindo wa kifudi fudi, maarufu kama “Kifo cha Mende”. Wanaume wanapenda wanawake, ambao ni wataalam kitandani. Wanaume wanapenda wanawake, ambao wanajiamini na wanabuni manjonjo mbalimbali wakati wa shughuli. Kama unataka kumridhisha mwanaume wako kitandani, basi soma mbinu mbalimbali, ambazo zinatumiwa na wapenzi mbalimbali.
#3 Fanya mazoezi na onekana Bomba. Wanaume ni watu wakujali sana muonekano wa mwanamke. Kwahiyo, sio lazima kuonekana kama walimbwende wa vichupi, lakini mtazamo wa karibu na hapo, utakuongezea mvuto zaidi kitandani. Ndio, mwanaume wako “anakupenda kama ulivyo” na tila lila nyingiiiii…..lakini lazima tuukabili ukweli kwamba watu wenye kufanya mazoezi wanaonekana na mvuto zaidi, hakuna kupinga hilo. Hata kwetu Bongo katika nyakati hizi za utandawazi, wakina kaka wengi wanawaona wanawake kama wakina Naomi Campbell na Jennifer Lopez, ambao wanatamani kuwa nao. Lakini hauhitaji kuwa kama wakina Naomi na Jennifer kumridhisha mwanaume wako, bali hakikisha tu upo katika umbo zuri la kumpelekesha kirahisi kitandani, Basi!
#4 Kuwa Mchokozi. Hapa haimaanishi ule uchokozi wa kuleta ugomvi, lahasha! Bali, ni ule uchokozi, ambao kwa lugha ya kingereza unafahamika kama “Tease”, kwa maana hiyo basi tunasema “Tease him”. Cheza nae michezo mbalimbali na burudika nae ipasavyo, na michezo isiwe ya kitandani tu, kama karata na kadhalika, bali michezo ya hata nje ya kitanda kama kukimbia na kucheza kidali po! Kama unataka kuwa mjuzi kitandani, basi unatakiwa umfanye mwanaume wako akutake wakati wote na popote pia. Kujamiiana sio kitasa ambazo unawasha na kuzima mnapokuwa chumbani tu. Mchokoze chokoze wakati mnasakata muziki jukwaani, na mchokoze chokoze (katika mitindo ya kimahaba, bila kuvuka mipaka) wakati yupo na marafiki zake.
#5 Jiamini na Jipende. Ndio, utaonekana vizuri zaidi ukipunguza maunene, lakini hiyo haimaanishi kwamba haupo bomba. Hakuna kinacho kera wanaume, kama mwanamke, ambae anauonea aibu mwili wake mwenyewe wakati anafanya mapenzi. Jiamini kuhusu mwili wako wakati upo mtupu, na jaribu mambo mbalimbali na mwanaume wako.
Usikose muendelezo wa sheria 5 za mwisho juma lijalo………………………….