Wednesday, January 25, 2017

HATUA 3 ZA KUBADILI TABIA INAYOKUKWAZA KATIKA MAHUSIANO

Kati ya kitu ambacho kinasumbua wengi na kimekwamisha wengi ni tabia.Wengi wana huzuni ndoa zimewashinda,kazi zimewashinda,fedha na mafanikio vimewakimbia,watoto wamewashinda,hawana marafiki hata miili yao haina afya kwa sababu ya tabia tu.
Wengine wamejiona ni kama wana laana,wengine wanafikiri labda wanaugua ugonjwa flani lakini shida siyo shida nitabia zao tu.
Hebu tuone namna gani tunaweza badilika au kubadilisha tabia zetu.

Tafuta Kujijua Binafsi:
Jiulize kwa nini umekuwa ukikwama mara kwa mara katika eneo  flani kama vile:-

(a)Kwanini haudumu ktk mahusiano ya kirafiki au ya mapenzi.
(b)Kwanini umeshindwa kufanikiwa kimaisha.
(c)kwanini watu wanakuchukia.
(d)kwanini hau-dumu kwenye kazi.
Unaweza pia kumuuliza mtu unaye mwamini akwambie jinsi ulivyo.

Chukua Hatua Kubadili Tabia:
Anza kufanya kinyume na ulivyokuwa umezoea kwa maana ya kwamba yale ambayo ni mazuri sasa. Zingatia haya:-
(a)Wataalam wa mambo wanasema ili jambo liwe tabia linafaa kufanya kwa siku “21” bila kuacha  baada yah apo jambo hilo litakuwa tabia.
(b)Ikikubidi kubadilisha mazingira ambayo unahisi ndiyo yamekuharibia tabia badisha hata kama itakugharimu.
(c)Ikikubidi kubadili marafiki ambao wamekuwa wakikushauri vibaya achana nao tu utapata marafiki wengine.
Majumuisho
Kumbuka haya:
(a)Tabia inaundwa au inatengenezwa na tabia ya mtu inamtegemea mtu mwenyewe na maamuzi yake.
(b)Tabia yako inaweza kukukwamisha kabisa katika Maisha yako yote au kukufanikisha katika mambo yote.
(d)Tabia yako itakutenga na watu au itakuunganisha na watu.
SASA UAMUZI NI WAKWAKO KUTENGENEZA TABIA YAKO ILI WATOTO WAKO WAIGE MEMA KUTOKA KWAKO.

No comments:

Post a Comment